MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI YAPUNGUA NCHINI


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Suzan Kolimba (Mb) akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI (UNAIDS), Bw. Dr. Leo Zekeng ofisini kwake jijini Dar Es Salaam leo. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Zekeng alisifu jitihada zinazofanywa na Tanzania katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa ukimwi ambazo zimesaidia kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo kwa asilimia 25 na pia idadi ya watoto wanaozaliwa na virusi vya ukimwi imepungua kwa kiasi kikubwa. Dkt. Zekeng alisema kuwa kutokana na mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS, Bi Michel Sidibe anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini mwezi Oktoba 2017 .
Dkt. Zekeng akionesha takwimu zilizopo katika ripoti ya UNAIDS zinazoonesha namna maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI yalivyopungua nchini Tanzania. 
Mazungumzo yanaendelea 
Mhe. Naibu Waziri akiagana na Dkt. Zekeng baada ya kukamilisha mazungumzo yao 
Picha ya pamoja