Ujenzi wa Daraja la Mto Momba Kuanza Mwaka Huu
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akielekea kukagua sehemu ambapo
litajengwa Daraja la Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe
.Kulia ni Meneja wa Wakala wa barabara (TANROADS)Mkoa wa Rukwa Eng.
Msuka Mkina na Wa pili kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Kwela Mhe. Ignas
Malocha.
Meneja wa Wakala wa
barabara(TANROADS), Mkoa wa Rukwa Eng. Msuka Mkina (aliyenyoosha
kidole) akimwonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng.
Edwin Ngonyani (Wa tatu kulia) eneo lipakapojengwa Daraja la Momba
wakati alipokagua sehemu ambapo litajengwa Daraja hilo litakalounganisha
Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Mbunge wa Jimbo la Kwela Mhe.
Ignas Malocha (Kulia) akifafanua jambo kwa wananchi wa kijiji cha
Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa wakati Naibu Naibu Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani alipotembelea
jimboni kwake.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (aliyenyoosha mkono) akifafanua kwa
wananchi wa kijiji cha Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa kuhusu
ujenzi wa daraja la Mto Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na
Songwe.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (Kulia) akitoa maelezo kwa wananchi
wa kijiji cha Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa kuhusu ujenzi wa
daraja la Mto Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Wananchi wa kijiji cha
Kilyamatundu kata ya Kipeta Mkoani Rukwa wakifurahi mara baada ya Naibu
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani (hayupo
picha) kutoa tamko la kupatikana kwa Mkandarasi atakayejenga daraja la
Mto Momba litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
Muonekano wa Sehemu ambapo daraja la Mto Momba litakapojengwa. Daraja hilo litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe.
…………………………………………………………………………..
Naibu waziri wa Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani amesema daraja la Mto Momba lenye
urefu wa mita 75 litakalounganisha Mkoa wa Rukwa na Songwe litaanza
kujengwa mapema mwaka huu.
Eng. Ngonyani ametoa kauli hiyo
mara baada ya kukagua barabara ya Kasansa hadi Kilyamatundu na eneo
litakapojengwa daraja la Momba na kusema kuwa Serikali imeshampata
Mkandarasi atakajenga daraja hilo.
“Serikali imeshatoa kiasi cha sh.
Bilioni tatu fedha hizo zimetusaidia kutangaza zabuni na kumpata
mkandarasi, tayari Mkandarasi wa ujenzi huu ameshapatikana na mkataba wa
makubaliano ya ujenzi umeshakamilika hivyo mkandarasi atausaini rasmi
hivi karibuni,” amesema Eng. Ngonyani.
Aidha, Eng.Ngonyani amemtaka
Meneja Wa Wakala wa barabara (TANROADS) Mkoa wa Rukwa kuhakikisha anatoa
ajira kwa wakazi waliopo kata ya Kipeta ambapo ujenzi wa daraja hilo
utafanyika.
Naye Mbunge wa Jimbo la Kwela
Mhe. Ignas Malocha ameishukuru Serikali ya awamu ya tano ya Mhe. Dkt.
John Magufuli kwa kutekeleza ahadi ya ujenzi wa daraja hilo ambalo
kukamilika kwake kutawaletea maendeleo wakazi hao kwa vile litaufungua
Mkoa wa Rukwa na kuunganisha na Songwe na Katavi.
“Kukamilika kwa ujenzi wa daraja
hili kutarahisisha usafirishaji wa mazao ya biashara kutoka mkoa wetu
kwenda mikoa mingine inayopakana na mkoa huu na kuokoa maisha ya
wananchi ambapo awali walikuwa wa wakiliwa na mamba na wengine kusombwa
na maji wakati kuvuka kwenye mto huu,” amesisitiza Malocha.
Kwa upande wake meneja wa
TANROADS Rukwa Eng. Msuka Mkina amewahakikishia wakazi kijiji cha
Kilyamatundu kuwa Wakala utasimamia ujenzi huo ili ukamilike kwa wakati
na viwango na kupitia mradi huo wananchi hao watapata ajira.
“Naomba niwahakikishie wakazi wa
hapa kuwa daraja hili sasa litaaanza kujengwa na nyinyi mtakuwa sehemu
ya wafanyakazi katika ujenzi wa mradi huu nawaomba mtoe ushirika kwa
mkandarasi pindi mradi huu utakapoanza,” amesema Eng. Mkina.
Naibu Waziri Eng. Edwin Ngonya
amekamilisha ziara yake ya kukagua ya kukagua Miundombinu ya barabara,
Viwanja vya Ndege, Ujenzi wa Nyumba za viongozi, huduma za mawasiliano
ya simu, Bandari na Madaraja katika Mkoani Rukwa.
Post a Comment