Hospitali Teule ya Mkoa wa Geita yapongezwa

KISIGINO HABARI

gey1
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na watoto Ummy Mwalimu akiongea na watoa huduma kwenye hospitali teule ya rufaa ya Mkoa wa Geita wakati alipofanya ziara ya kikazi katika hospitali hiyo ambapo aliridhishwa na huduma zitolewazo na hospitali hiyo na kuwapongeza kwa kuanzisha kitengo cha ubora za huduma za faya ambacho kinasaidia kuimarisha afya ya wagonjwa ikiwemo mama na mtoto pamoja na lishe.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga na nyuma ya Waziri ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Geita Thomas Dimme.

gey2
Waziri Ummy akimjulia hali akina mama waliojifungua katika wodi ya Wazazi.Akina mama hao walikiri kuhudumiwa vizuri na watoa huduma hiyo pia hawajatozwa fedha yeyote kama sera ya afya inayosema kila mama mjamzito matibabu ni bure
gey3
Mhudumu wa afya pekee wa kike katika chumba cha kuhifadhi maiti Bi.Angela Milinga(mwenye koti jeupe) ambaye anafanya kazi katika hospitali hiyo akimshukuru Waziri Ummy kwa kufika katika kitengo chake na kujionea jinsi wanavyofanya kazi .
gey4
Mhudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti Bi. Anjela akieleza jinsi anavyofanya kazi kwa Mhe. Waziri (hayupo pichani) mara baada ya kutembelewa na ugeni huo.
gey5
Watumishi wa hospitali hiyo wakimsikiliza Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto(hayupo pichani) wakati wa mkutano wa ndani mara baada ya kutembelea sehemu mbalimbali za kutolea huduma za hospitali hiyo
gey6
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita,Dkt. Joseph Kisala akisoma taarifa ya hospitali hiyo,Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Geita mjini Mhe.Costantine Kanyasu na Kushoto ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Brian Mawalla
gey7
Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo Dkt. Brian Mawalla akimfafanulia jambo Waziri wa afya(hayupo pichani) wakati wa mkutano na watumishi wa hospitali hiyo
gey8
Picha ya Pamoja ya Waziri Ummy Mwalimu, Viongozi wa Mkoa,Wilaya na watumishi wa hospitali hiyo mara baada ya kumaliza mkutano wa ndani.Katika kikao hicho Waziri aliwataka wafanyakazi ambao hawataki kubadilika na kuwajibika wakati wa kuwahudumia wagonjwa  wapishe kwani hivi sasa kuna wahitimu wengi wanahitaji ajira Serikalini hususan kada ya afya(Picha zote na Wizara ya Afya)