TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA


index

taarifa ya jeshi la polisi mkoa wa mwanza kwa vyombo
vya habari leo tarehe 10.08.2017

·         watu wawili wamefariki dunia na mwingine mmoja kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari na bajaji wilayani kwimba.

·         mtu mmoja anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana na noti bandia za elfu kumi 20 zenye thamani ya tsh 200,000/=, wilayani sengerema.

kwamba tarehe 09.08.2017 majira ya saa 21:00hrs katika barabara ya ngudu kwenda hungumalwa eneo la kitongoji cha mwalugunda kijiji na kata ya nyamilama  wilaya ya kwimba mkoa wa mwanza, gari namba t.355 arz aina ya mistubishi fuso likitokea ngudu kwendwa hungumalwa likiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la muro robart, miaka 35, mkazi wa mkoa wa kilimanjaro liligonga bajaji ya magurudumu matatu yenye namba t.675 buf iliyokuwa ikitokea hungumalwa kwenda ngudu ikiendeshwa na dereva aitwaye kulwa philimon @ fulano miaka 50, mkazi wa kijiji cha nhaniga, na kusababisha vifo kwa 1.kulwa philimon @ fulano dereva bajaji, 2.jina bado halijafahamika, abiria wa bajaji, na kusababisha majeruhi kwa edward dornad miaka 42, abiria wa bajaji, mfanyabiashara, mkazi wa nyamilama.
inadaiwa kuwa majira tajwa hapo juu dereva wa bajaji alikuwa akitokea maeneo ya hungumalwa akielekea ngudu huku akiwa amebeba abiria wawili lakini bajaji yake ilikuwa haina taa  na kutokana na bajaji hiyo kukosa taa dereva wa bajaji hiyo inasemekana alikuwa akitumia tochi aliyokuwa ameifunga kifuani kama taa, ndipo alipofika eneo hilo tajwa hapo juu dereva wa gari alishindwa kutambua ujio wa bajaji na kupelekea kugongana na kusababisha vifo vya watu wawili tajwa hapo juu na majeruhi, ambapo dereva wa gari baada ya jali kutokea alitoroka eneo la tukio, juhudi za kumtafuta bado zinaendelea.
uchunguzi wa awali unaonesha chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa bajaji kuendesha chombo cha moto barabarani bila ya taa  na kupelekea ajali hiyo kutokea na kupelekea vifo na majeruhi. majeruhi amelazwa hospitali ya wilaya ya ngudu akiendelea kupatiwa matibabu na hali yake inaendelea vizuri, miili ya marehemu pia imehifadhiwa hospitalini hapo kwa ajili ya uchunguzi, pindi uchunguzi ukikamilika itakabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi.
kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa wito kwa wakazi wa jiji na mkoa wa mwanza hususani waendeshaji wa vyombo vya moto akiwataka kuchukua tahadhari pindi wawapo barabarani huku wakizingatia sheria, kanuni na taratibu za usalama barabarani ili kuepusha ajali na vifo vinavyoweza kuepukika.
katika tukio la pili,
mnamo tarehe 09.08.2017 majira ya saa 14:00hrs katika kijiji cha kanyara kata ya bulyaheke tarafa ya buchosa wilaya ya sengerema mkoa wa mwanza, fabian jackson miaka 32, mkazi wa mahina mwanza, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kupatikana akiwa na noti bandia 20 za elfu kumi zenye thamani ya kiasi cha tsh 200,000/=, kitendo ambacho ni kosa la jinai.
awali polisi wakiwa kwenye doria na misako walipokea taarifa kwamba katika kijiji cha kanyara yupo mtu ambae ameingia kijijini hapo lakini ana noti bandia nyingi. aidha baada ya askari kupokea taarifa hizo walifanya ufuatiliaji wa haraka hadi kijijini hapo na kufanya upelelezi na msako wa kumtafuta mtu huyo 
ndipo baadae walifanikiwa kumtia nguvuni mtuhumiwa akiwa na kiasi hicho tajwa hapo juu cha noti hizo bandia.
polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa kuhusiana na tukio hilo pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani. aidha msako wa kuwatafuta watu wengine wanaoshirikiana na mtuhumiwa katika utengenezaji wa noti bandia bado unaendelea.
kamanda wa polisi mkoa wa mwanza naibu kamishina wa polisi ahmed msangi anatoa rai kwa wakazi wa mkoa wa mwanza, akiwataka kuacha tabia ya kutengeneza noti bandia kwani ni kosa la jinai na endapo mtu akikamatwa hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. aidha pia anaendelea kuwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuweza kudhibiti uhalifu katika mkoa wetu.
  
imetolewa na;
dcp: ahmed msangi
kamanda wa polisi (m) mwanza