MANISPAA YA ILALA JIJINI DAR' YAONGOZA KITAIFA MCHEZO WA WANAFUNZI WASIOONA { GOLBO}

Mmoja wa wanafunzi akikabidhi tuzo ya kombe ambalo walipata kuchukua ushindi kwa Meya wa manispaa ya ilala jijini Dar hivi leo wa kwanza kushoto ni Naibu meya wa manispaa hiyo Omary kumbilamoto,pamoja na Afisa elimu Msingi wa Manispaa hiyo Bi Elizabeth Thomasi na aneyefuata ni katibu tawala wa manispaa hiyo Edward Mpogolo

Mmoja wa waalimu ambae amekuwa ni mlezi wa wanafunzi huo akikabidhi zawadi ya Tuzo ya kombe kwa Meya wa manispaa ya ilala jijini Dar es salaam
 Zawadi za Kombe zikiendelewa kukabidhiwa kwa manispaa hiyo ya ilala likiendelea
 Haya ndiyo makombe yaliyokabidhiwa kwa manispaa ya ilala kama yanavyoonekanawa kwanza kushoto ni Naibu meya wa manispaa hiyo Omary kumbilamoto,wa pili kushoto ni Meya wa manispaa hiyo pamoja na Afisa elimu Msingi wa Manispaa hiyo Bi Elizabeth Thomasi na aneyefuata ni katibu tawala wa manispaa hiyo Edward Mpogolo

Baadhi ya waalimu pamoja na wanfunzi wakifurahia mara baada ya kukabidhi makombe hayo kwa manispaa ya ilala
 Hawa ni baadhi ya madiwani pamoja na watendaji mbalimbali walipo katika ukumbi wa mikutano kwa ajili ya kikao chao cha baraza kujadili maendeleo ya wilaya wakishudia kukabidhiwa kwa makombe hayo kwa manispaa yao
                     
Manispaa ya ilala hivi leo imepokea  tuzo za kombe toka  kwa wanafunzi waliofanya vyema katika mchezo wa GOLBO ukiwa ni mchezo maalumu kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa macho kutoka katika shule ya uhuru mchanganyiko iliyopo katika manispaa ya ilala jijini Dar es salaam.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi makombe kwa ajili ya wanafunzi hao waliofanya vizuri katika mchezo huo Meya wa manispaa ya ilala Charles Kuyeko ambae pia siku ya leo ndie mwenyekiti katika kikao kinachoendelea cha baraza la madiwani wa manispaa hiyo amesema kuwa wao kama madiwani wa manispaa ya ilala wanapenda kutoa pongezi nyingi hasa kwa wanafunzi,waalimu pamoja na maocha wao wa kimchezo hasa kwa kuwa saidia wanafunzi hao hadi kuweza kuinuka kidedea katika mashindano hayo.

Hakuishia hapo bali alizidi kuisihi halmashauri nyingine pamoja na shule nyingi za hapa nchini kuhakikisha wanaweka mbele zaidi swala la elimu kwa wanafunzi kwani huwa saidia katika kuboresha utendaji wao wa kimasomo hasa wanafunzi wenye uhitaji maalumu kutoachwa bali waendelezwe kwa michezo mbalimbali kama hii waliyoweza kuiletea wilaya ya ilala ushindi.

Naye Afisa Elimu msingi wa manispaa hiyo ambaye pia ni kaimu mkurugenzi kwa niaba ya mkurugenzi wa ilala  amesema katika mipango yake ya awamu hii kwa manispaa ya ilala ni katika kuhakikisha anaweka wigo mpana zaidi wa kielimu pamoja na kuhakikisha sekta ya uwajibikaji kwa watumishi wote ngazi ya elimu msingi kwa manispaa hiyo watajitahidi kufanikisha swala la elimu bora michezo bora pamoja na uwajibikaji bora kwa utendaji wa kiwilaya.

Huku akitoa ufafanuzi kwa mchezo huo wa GOLBO kwa wanafunzi hao wasioona kwa kusema huwa wanakuwa na mipira yao muhimu ambayo kwa ndani inakuwa na kengele hivyo mwanafunzi anapokuwa anacheza husikiliza mlio wa kengele na kufahamu ni wapi unapoelekea mpira huo.

Mchezo huo ambao pia wanafunzi hao walipata kucheza na wachezaji kutoka timu ya Everton pindi walipofika hapa nchini na kuamua kufanya ziara yas kutembelea katika shule ya wanafunzi wenye ulemavu maalumu  wa shule ya uhuru mchanganyiko na kuonyesha umahiri wao.