WAKENYA WATATU WAHUKUMIWA KIFO KWA KUMVUA MWANAMKE NGUO

Wabanawake wa Kenya waandamana kupinga udhalilishwaji unaotekelezwa na baadhi ya makundi ya watu yanayopinga jinsi walivyovalia nguo zao.
Mahakama moja ya Nairobi, siku ya Jumatano iliwahukumu wanaume watatu kunyongwa, baada ya kupatikana na hatia ya kumvua nguo mwanamke mmoja, kumdhalilisha na kujaribu kumbaka.
Kisa hicho kiltokea wakati wa wimbi la uvamizi wa wanawake miaka mitatu iliyopita, ambapo makundi ya watu yalikuwa yakidai kwamba wanawake walikuwa wanavaa mavazi yasiyokubalika.
Watu hao watatu walipatikana nahatia ya wizi wa kutumia nguvu, ambao hukumu yake ni kifo.
Hata haivyo, sheria ya hukumu ya kunyongwa nchini Kenya haijatekelezwa tangu mwaka wa 1987, na hukumu kama hizo zimebadilishwa na kuwa vifungo vya maisha.
Baadhi ya visa vya uvamizi huo, ambavyo vilikithiri mnamo mwaka wa 2014 vilirekodiwa kwanye simu za mkono, na kupelekea maandamano, huku waliokuwa wakipinga vitendo hivyo - wengi wao wakiwa wanawake - wakianzisha hashtag iliyoitwa #MyDressMyChoice kwenye mitrandao ya kijamii.
Muathiriwa huyo aliiambia mahakama kwamba wanaume hao watatu walikuwa kati ya kundi la wanaume saba waliotaka kumbaka ndani ya basi, lakini wakakaachana naye alipowaambia kwamba alikuwa na virusi vya ukimwi.