NDEGE ZA KUTOKA SAUDI ARABIA HADI MAREKANI ZAONDOLEWA MARUFUKU YA LAPTOPS
Marufuku ya laptopu
ndani ya ndege zinazofanya safari ya moja kwa moja kutoka nchini Saudi
Arabia hadi Marekani imeondolewa, kwa mujibu wa shirika la ndege la
Saudi Arabian.
Linasema kuwa viwanja vya ndege ambavyo ndege zinazoelekea Marekani hutumia, vimeruhusiwa na idara ya ulinzi ya Marekani.
Uwanja wa King Khalid mjini Riyadh ndio wa mwisho kati ya viwanja kumi vilivyoondolewa marufuku hiyo.
Mwezi Machi Marekani ilipiga marufuku laptopu na vifaa vingine vikubwa vya elektroniki kutoka nchi nane za kiislamu.
Mashirika ya Kuwait Airways na Royal
Jordanian yamekuwa ya hivi punde kuruhusu abiria kubebea laptopu ndani
ya ndee zinazoelekea Marekani.
Mashirika hayo mawili yalisema
yameshirikiana na maafisa wa Marekani kuimarisha usalama kwa ndege
zinazotoka nchini Kuwait na Jordan.
Marekani ilitangaza marufuku
hiyo mwezi Machi kwa safari za moja kwa moja kutoka nchi nane za
kiislamu kutokana na hofu kuwa mabomu yangebebwa ndani ya vifaa hivyo.
Mashirika ya ndege ya Etihad, Turkish Airlines, Emirates and Qatar yaliondolewa marufuku hiyo wiki iliyopita.
- Marekani yapiga marufuku laptopu na tabiti kutoka mataifa 8
- Uingereza yapiga marufuku laptopu ndani ya ndege kutoka nchi 6
- Marekani yazuia abiria kubeba laptopu kutoka Misri na Morocco
Shirika la Royal Jordanian ambalo hufanya safari katika miji
mitatu ya Marekani kutoka Amman, mji mkuu wa Jordan, liliondoa marufuku
hiyo baada ya hatua mpya za kiusalama zilizochukuliwa kwenye ndege
zinazoelekea nchini Marekjni.
Shirika linalomikiw na serikali la
Kuwait Airlines ambalo hufanya safari zake kutoka Kuwait kuenda mjini
New York likipitia Ireland lilisema kuwa marufuku hiyo ilitolewa baada
ya maafisa wa Mareknian kukagua usalama kwenye safari zake
Viwanja wa King Abdulaziz mjini Jeddah na King Khalid mjini Riyadh
vyote vimekaguliwa na kuruhusiwa laptopu kuingia viwanjani humo.
Viwanja hivyo viwili vinatumiwa na ndge zinazosafiri moja kwa moja kutoka Saudi Arabia kwende Marekani.
Shirika
la ndege la Saudi Arabian ambalo pia linajulikana kama Saudia ndilo
pekee ambalo hufanya safari za moja kwa moja kuenda Marekani.
Post a Comment