Kenyatta atangaza vita kamili na al-Shabaab
Rais Uhuru Kenyatta ametangaza operesheni kabambe ya kuwamaliza al-Shabaab.
Akizungumza Jumatatu huko Kizingitini, Kaunti ya Lamu, Rais ameagiza kuwa magaidi wauawe na kuzikwa.
“Tutawamaliza magaidi wote,” amesema kwani magaidi hao wameugeuza
msitu wa Boni ni mahali pa mchezo mchafu, ambapo wamekuwa
wakiwashambulia na kuua wakazi wa eneo hilo kabla ya kutokomea katika
msitu huo.
Vyanzo vya habari nchini Kenya vimesema Rais ambaye alionekana akiwa
na hasira katika hotuba yake ambayo iliashiria pia kuwa kutekwa nyara
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mariam El Maawy na magaidi hao wiki
iliopita, na kupigwa risasi na kujeruhiwa, inawezekana alilengwa kwa
sababu ya kutoa hati kwa wananchi wa eneo hilo.
Maawy aliokolewa na Jeshi la Ulinzi la Kenya baada ya wapiganaji hao
wa al-Shabaab kuteka gari yake kabla ya kumuua mlinzi wake, dereva na
mpwa wake. Watu wengine wawili walipoteza maisha katika tukio hilo.
Post a Comment