Mjadala wa Lissu ufungwe
Mkuu wa jeshi la polisi nchini, IGP Simon Sirro ametaka mjadala ufungwe mara moja kuhusu
sakata la mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu kupigwa risasi na watu wasiojulikana mnamo
Septemba 7, 2017 akiwa mjini Dodoma.
IGP Sirro ametoa kauli hiyo leo akiwa ziarani jijini Mbeya wakati akizungumza na vikosi vya
ulinzi na usalama ambapo amewaonya wanasiasa kuacha kuuendeleza mjadala wa jambo hilo
na waliachie jeshi la polisi lifanye kazi yake.
Mbali na hilo IGP Sirro amewataka wananchi hususani wa mkoa wa Mbeya, kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi na badala yake kutii sheria bila shuruti na kwamba, Jeshi la Polisi
litahakikisha linawachukulia hatua kali za kisheria ili kukomesha tabia hiyo.
Aidha Sirro amedai kuwa takwimu za uingizwaji na utumiaji wa dawa za kulevya imepungua kwa
kiasi kikubwa kutokana na kufanyika kwa operesheni za mara kwa mara zinazofanywa na Jeshi hilo
la polisi.
Post a Comment