RC MAKONDA AZIAGIZA MANISPAA ZA MKOA HUO KUTENGA MAENEO YA WAJASILIAMALI


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda Akizindua Majengo na ujenzi wa Viwanda vidogo vidogo. 

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, leo meweka jiwe la msingi na kuzindua Majengo mawili ya wajasiriamali  mali wa Wilaya ya Kinondoni  yaliyijengwa katika eneo la karakana Mwananyamala.

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe. Makonda amewataka wajasiliamali kutumia fedha wanazokopeshwa kwa kuendeleza shughuli zao za kibiashara  na kuita katika manispaa zote za Mkoa huo kutenga na kujenge maeneo ya
  wajasiliamali wanaokopeshwa, amewaelekekeza watendaji wa jiji kuwa weka wajasiriamali  katika kituo kimoja katika kila wilaya.

Amesema Rais Magufuli akianza ziara katika mkoa huo, atamkutanisha na wajasiliamali mali wa mkoa ili waonyeshe bidhaa zao  na amesisitiza tiza wa matchinga kuuza bidhaa za ndani ili kukuza uchumi wa nchi, naataandaa maonyesho katika  viwanja vya mnazi moja kila mwezi.

"nawaelekeza Manispaa zote kutengeza maeneo ya wajasiliamali mali ili hao wanaokopeshwa waweze kulipa mikopo bila  usumbufu maakipindi cha nyuma walikopeshwa hawaonekani wako wapi kwahao itakuwa rahisi hata kuwa ona walipo.”

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Paul Makonda akiagana bidhaa za wajasiriamali wa mkoa wa Dar es Salaam, mwananyala leo hii. 
Hatahi ameitaka Halmashauri ya jiji kuendesha vizuri soko la kariakoo kwa kuwa sasa linajiendesha kwa hasara,

"sisi viongozi tunapofanya Uchunguzi na maamuzi hasa tunaomba mwambie Mungu naomba mtu amini, nilipoundakamati kuchunguza hili hawakunielewa lakini sasa mapato yameongezeka nadhani sasa hatanikikupa ninyi Madiwani mnaionafaida" alisema Makonda.

Aidha amewataka wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam kushikamana na kumuunga mkono Rais Magufuli  ili kulinda rasilimali za nchi, Kuna watu wabaya wanatuonea wivu wanaweza kutuchochea tupigene.

Kwa upande wake Naibu meya wa jiji La Dar es salaam Musa Kafana amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Makonda kwa kutoa ushirikiano kwa mambo yote yanayofanyika katika Jiji hilo.

Ameongeza kuwa  Halmashauri ya jiji imetenga maeneo mbalimbali ya Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam  kwaajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo maeneo ya makaburi  kwa kuwa maeneo ya zamani yamejaa .

Naye Mkurugenzi wa jiji La Dar es salaam Sporadi  Liana amesema halmashauri ya jiji hilo imepanga malengo ya kuwajengea viwanda vidovidogo Wanawake na walemavu ambapo vitajengwa kutokana na fedha za asilimiakumi  ya mapato ya halmashauri ya jiji, nakuongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2016/2017halmashauri hiyo ili tena kiasi cha shilingi 200,000,000.00 kwaajili ya viwanda hivyo.

Amesema ,Katika awamu ya kwanza ya ujenzi huo miundombinu iliyo jenga ni Pamoja na Majengo ya viwanda vidogo vyumba vitatu Choo cha umma kimoja pamoja na lango la kuingilia Kiwandanihapo. Zaidi ya milio 

RC makonda ameweka jiwe la msingi may katika viwanda vidogo vidogo katika karakana ya jiji iliyopo mwananyamala dar es salaam.