Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, kuwahamishia wauza magari Kigamboni

Related image
TAZAMA VIDEO HII MPANGILIO WA KIGAMBONI MPYA.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amewataka wafanya biashara wa magari wa Dar es Salaaam kuhamia Kigamboni kwenye eneo Maalum lilitengwa kwa jili ya kufanyia biashara hiyo.

Akiongea na mwanahabari wetu Mheshimiwa Makonda amesema kuanzia kesho wauza magari waende wakaripoti ofisini kwake na waseme wanahitaji square meta ngapi zitakazo tosha kwa ajili ya kuhifadhia magari yake.

Mheshimiwa Makonda aliongeza kwa kusema anataka kuliweka jiji la Dar es Salaam katika mpangilio maalum hivyo hakutakuwa na Yard ya Magari katikati ya Jiji hilo, alisema Duniani kote yard za madari ni kama viwanda vidogo hivyo hutengewa eneo maalum na siyo maeneo holela.

Chanzo: Kiganjanileo.blogspot