Wananchi wa Sumbawanga Mkoani Rukwa Wamepinga kujengwa Kwa Kiwanda Cha Kusindika Nafaka.
Wananchi hao wa kata hiyo wakiongea mbele ya mbunge wa Sumbawanga mjini
Mheshimiwa Aeshi Hilal, wamesema kiwanda hicho cha kusindika nafaka
kikianza kufanya kazi, kitaathiri mno hali za wagonjwa wanaopata huduma
kwenye zahanati hiyo, ikiwa pamoja na akina mama wajawazito wanaotegemea
kujifungua katika zahanati hiyo
.
.
Kutokana na hali hiyo wananchi hao wamepinga vikali ujenzi wa kiwanda hicho na kusema haupaswi kuendelea katika eneo hilo
Akizungumza na wananchi hao mbunge wa Sumbawanga mjini Mheshimiwa Aeshi
Hilal, amesema licha ya serikali ya awamu ya tano kuhimiza ujenzi wa
viwanda nchini, lakini ujenzi huo ni lazima uzingatie sheria na taratibu
zote za afya na mazingira kwa ujumla, na hasa ikizingatiwa kuwa
manispaa hiyo imeshatenga tayari maeneo ya uendelezaji wa viwanda.
Post a Comment